Nenda kwa yaliyomo

Kifinisia

Kutoka Wikipedia, kamusi elezo huru
Abjadi ya Kifinisia
Faili:Lamine Pyrgi.jpg
Mwandishi wa Kifinisia

Kifinisia ilikuwa lugha ya Kisemiti iliyozungumzwa kati ya 1100 KK hadi takriban 600 BK katika maeneo ya pwani la Kanaani na Shamu ya magharibi ambako leo hii kuna nchi za Israeli, Lebanoni na Syria.

Ilikuwa lugha ya Wafinisia ikaenea pamoja nao katika koloni zao hadi Afrika ya Kaskazini kama Karthago na Hispania.

Kifinisia ilikuwa lugha ya kwanza iliyoandikwa kwa aina ya alfabeti iliyoendelezwa baadaye katika alfabeti ya Kigiriki. Hali halisi mwandiko huu ulikuwa abjadi ukawa mama wa miandiko yote ya Kisemiti (kama herufi za Kiarabu na Kiebrania) na pia wa alfabeti zote zilizofuata alfabeti za Kigiriki na Kilatini.

pFad - Phonifier reborn

Pfad - The Proxy pFad of © 2024 Garber Painting. All rights reserved.

Note: This service is not intended for secure transactions such as banking, social media, email, or purchasing. Use at your own risk. We assume no liability whatsoever for broken pages.


Alternative Proxies:

Alternative Proxy

pFad Proxy

pFad v3 Proxy

pFad v4 Proxy