Content-Length: 77641 | pFad | http://sw.wikipedia.org/wiki/Bamba_la_Ufilipino

Bamba la Ufilipino - Wikipedia, kamusi elezo huru Nenda kwa yaliyomo

Bamba la Ufilipino

Kutoka Wikipedia, kamusi elezo huru
Ramani ya bamba la Ufilipino

Bamba la Ufilipino (ing. Philippine Plate) ni bamba la gandunia mojawapo lililopo chini ya bahari ya Pasifiki. Liko chini ya sehemu ya bahari iliyopo upande wa kaskazini-mashariki ya visiwa vya Ufilipino.

Upande wa mashariki wake Bamba la Pasifiki linasukumwa chini ya Bamba la Ufilipino. Mwendo huu umesababisha kutokea kwa mifereji ya bahari kama vile ya Bonin, Mariana, Yap na Palau. Mpaka na Mfereji wa Mariana kipande kimeanza kuvunjika na wakati mwingine hutajwa kama bamba la pekee kwa jina la Bamba la Mariana[1].

Upande wa kaskazini bamba hili linazamishwa chini ya visiwa vya Japani na hapa kugongana na Bamba la Ulaya-Asia. Hali hii ni sababu ya kutokea kwa mitetemeko ya ardhi mikali nchini Japani.


  1. Bird, P. (2003). "An updated digital model of plate boundaries". Geochemistry, Geophysics, Geosystems. 4 (3): 1027. doi:10.1029/2001GC000252.
  • Robert Hall, Jason R. Ali, Charles D. Anderson, Simon J. Baker: Origin and motion history of the Philippine Sea Plate. Tectonophysics, vol. 251, no 1–4, 1995, pp. 229–250, ISSN 0040-1951 doi:10.1016/0040-1951(95)00038-0








ApplySandwichStrip

pFad - (p)hone/(F)rame/(a)nonymizer/(d)eclutterfier!      Saves Data!


--- a PPN by Garber Painting Akron. With Image Size Reduction included!

Fetched URL: http://sw.wikipedia.org/wiki/Bamba_la_Ufilipino

Alternative Proxies:

Alternative Proxy

pFad Proxy

pFad v3 Proxy

pFad v4 Proxy